Latest News

Latest Posts

19 wauwa katika mlipuko Nigeria

- Friday, May 2, 2014 No Comments

Waliojeruhiwa walikimbizwa hosipitalini
Maafisa nchini Nigeria wanasema kuwa watu 19 wameuawa baada ya mlipuko kutokea katika kituo cha basi katika mji mkuu wa taifa hilo Abuja.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa idara ya kushughulikia mikasa na hali ya dharura- FEMA- Abbas G Idriss, watu 60 walijeruhiwa vibaya lakini sitaka kati yao wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani. Amesema kuwa magari sita yameharibiwa katika mlipuko huo.
Mlipuko huo umetokea katika eneo la Nyanya, karibu na kituo cha basi ambako zaidi ya watu sabini waliuwawa katika shambulizi la tarehe14 mwezi Aprili.
Ripoti za awali zimesema kuwa watu kadhaa wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Waandishi wanasema kuwa mlipuko huo umesababishwa na bomu lililotegwa ndani ya gari. Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho amesema aliona miili 20 ya watu waliouwawa. Hakuna kundi lililodai kuhusika katika shambulizi hilo lakini kundi la wanamgambo wa kiislamu la Boko Haram limewahi kutekeleza mashambulizi kama hayo mjini Abuja
Mengi ya mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakitokea katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Lakini shambulizi la bomu la tarehe 14 Aprili lilizua hofu kwamba huenda wanamgambo hao wameanza kupanua maeneo wanayoendeleza harakati zao.
 chanzo:BBC SWAHILI

Simba SC. yatinga Fainali kombe la Mapinduzi Zanzibar

- Friday, January 10, 2014 No Comments


Klabu ya Simba imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza fainali ya kombe la Mapinduzi baada ya kuifunga URA ya Uganda mabao 2-0.
mabao ya Simba kwenye mchezo huo yamefungwa na beki Joseph Owino pamoja na 
 
kiungo Amri Kiemba 
 huku kiungo Owen Kasule wa URA akilimwa kadi nyekundu kwa kumchezea madhambi Ramadhani Singano.
Simba sasa itacheza fainali siku ya Jumatatu Saa 10:00 Uwanja wa Amaan na timu ya KCC pia toka nchini UGANDA iliyoitoa AZAM kwa mabao 3-2.
 Kikosi cha Msimbazi leo kilikuwa:
Ivo Mapunda, Haruna Shamte, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’/William Lucian 'Gallas', Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Haroun Chanongo, Amri Kiemba/Said Ndemla, Ramadhani Singano ‘Messi’, Amisi Tambwe/Ramadhani Chombo ‘Redondo’ na Awadh Juma/Uhuru Suleiman. 
URA; Mugabi Yassin, Samuel Ssenkoom, Alan Munamba/James Kasibante, Mussa Doca, Jonathan Mugabi, Oscar Agaba, Augustine Nsumba, Owen Kasuule, Erisa Sekisambu/Ngama Emmanuel, Feni Ali/Milos Ilic na Hashimu Sempalia.

Official Trailer la Dhoom3

- No Comments
Hii Movie ni muendelezo wa story ambayo mara ya mwisho imechezwa na Hrithik Roshan (kwenye picha hii) mwaka 2006.
Safari hii imeendelezwa na mkali wa action Aamir Khan. Kiukweli hili ni Bonge la Movie na si la kukosa limeingia Sokoni trh.25/12/2013, ikiwa ni Wiki 3 baada ya Krrish 3 kutoka.

Mpoki na demu wa kizungu

- Monday, October 14, 2013 No Comments

Tazama Raaz2 Full movie with English Subtitle

- Tuesday, September 3, 2013 No Comments

diamond my number one official video

- Monday, September 2, 2013 No Comments

Timbulo - Sina Makosa.(Official Video)

- Monday, August 12, 2013 No Comments